Ijumaa 22 Mei 2026 - 00:30
Faradhi ya Tawhidi na kisiasa ya Hija haina maana bila ya kujitenga na washirikina

Hawza/ Mkurugenzi wa Hawza za Wabahrain walioko Iran ameelezea “kuwambali na washirikina” kuwa ni msingi wa Qur’ani na akasisitiza: Hija ni faradhi ya Tawhidi na ya kisiasa, na kama alivyosema Imam Khomeini, Hija bila ya kujitenga na washirikina haina maana.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Abdullah al-Daqqaq, mwalimu na mkurugenzi wa Hawza ya Wabahrain wanaoishi Qum Iran, na mwakilishi wa Ayatullah Issa Qassim kutoka Bahrain, katika kikao maalumu cha “Hija; Mahali pa Miadi ya Umoja” kilichofanyika Jumatano kwa juhudi za Majma' al-'Alami li-Taqrib al-Madhahib al-Islamiyyah, alisema: Msingi wa kujitenga na washirikina ni miongoni mwa mambo ambayo Imam Khomeini aliyasistizia, na alisema kwamba, Hija bila ya kujitenga na washirikina haina maana.

Sheikh al-Daqqaq katika kikao hiki kilichofanyika sambamba na kuwadia kwa siku za Hija ya Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu, alisisitiza: Msingi wa kujitenga na washirikina katika Qur’ani Tukufu umeelezwa mwanzoni mwa Suratut-Tawbah; Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Suratut-Tawbah anasema:

"Na watangazie watu Hija; watakujia kwa miguu na juu ya kila ngamia aliye konda, wakija kutoka katika kila njia ya mbali".

Aliongeza: Katika aya hii, “أَذَانٌ مِنَ اللَّهِ” maana yake ni tangazo kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kwa watu katika siku ya “Hija Kubwa”, kwamba Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wamejitenga na washirikina.

Al-Daqqaq alikumbusha kuwa: Hija, Tawafu na Sa’y ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee; hivyo muumini hutekeleza ibada za Hija kwa ajili ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu. Tawhidi hii katika ibada ina matawi mawili: upande wa kuthibitisha na upande wa kukataa, ambao ni kuikanusha shirki na washirikina kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Alisisitiza kuwa: Hija ni ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na ni lazima itangaze upande wa kukataa; yaani kuikanusha shirki kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kuthibitisha kwamba umoja, uungu, uja na uumbaji ni wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hivyo Tawhidi ya ibada, Tawhidi ya umoja, na Tawhidi ya ulezi hupatikana; yaani hakuna mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, hakuna Mlezi isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna Muumba isipokuwa Mwenyezi Mungu.

Al-Daqqaq aliongeza kusema: Kwa hiyo Hija inaashiria faradhi ya Tawhidi, ya Kiungu na ya kisiasa, na kuhifadhi upande wa kiibada huku upande wa kisiasa — ambao ndani yake kuna kujitenga na washirikina na kujitenga na ubeberu wa kimataifa — ukipuuzwa, hakuna maana yake.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha